1. Hifadhi yake
2. Balehe, utu uzima na mvuto
3. Onyo la mama
4. Hatari ya kujitolea
5. Wanaume wote si waovu
Hifadhi ya msichana ni jambo kubwa, hasa ipasapo mwanamume kutoa shauri. Walakini bahari kuu huvukwa. Kwa hivi ninatumaini kuwa sitazama katika jaribu hili.
Msichana wa leo ni mama wa kesho. Upumbavu ulioje kujifanya hatudhuriwi na mambo yake! Ukitaka kukomesha maisha yetu ua wasichana, na baada ya miaka si mingi hapatakuwa na kitu kiitwacho mtu. Robo tatu za hifadhi hii lazima, zifanywe na wanaume.
Msichana akipita balehe akafikia utu uzima hufanya mvuto mkubwa kwa mwanamume. Mvuto huu ni maumbile, na pana watu wadaio hapana maana ya kugombana na maumbile. Nataka ningeona kama waonavyo wenzangu; lakini watu wote hawana vipawa namna moja. Kinyume cha maono yao, naona halali kugombana na tokeo hili kwa sababu pengine mvuto huu humponza msichana.
Kama yapasa msichana kujitafutia riziki kwa utumishi kama uyaya, uuguzaji au ualimu; tena kama akikaa pasipo wazazi wake hukutana na majaribu mengi ya wanaume. Vikundi vya wanaume humzunguka kama nzi kando ya kipande cha sukari. Humganda kama nyuki juu ya tone la asali.
Kwa msichana aliyelelewa vema majaribu haya hayadhuru. Onyo la busara la mama likitolewa mapema ni ngao bora kwa msichana kuliko buibui jeusi, dirisha la komeo au mlango wa kufuli. Kwa bahati mbaya wasichana wengi hawapati malezi mazuri. Hawa lazima waokolewe. Wakiokoka watasaidia kuhimiza majilio ya Afrika bora. Hatutaki Afrika kuwa bora?
Msichana akijitolea ovyo katika tamaa ya mwili huharibikiwa na mambo yake mengi. Huingia katika hatari ya maambukizo ya maradhi mabaya. Hasara nyingine ya kusikitisha ni uzazi wa haramu. Kwa hali ya kiitikadi iliyo katika maisha yetu ya sasa, ni dhiki kubwa kwa msichana kupata mtoto asiye baba wa kusaidia ulezi wake. Moja lolote katika haya likitokea huharibu heshima ya msichana. Hufukuzwa kazini, hapati arusi njema na dunia nzima humdharau. Matokeo haya mabaya sana, nayo yote huletwa na wanaume wajinga na walafi.
Isifikiriwe kuwa wanaume wote waovu. Hasha mara mia. Wanaume wengi wema nao wana heshima. Hawana nia ya kuharibu maisha ya msichana hata kidogo. Fahari yao kubwa katika maisha ni kuwasaidia.
To save this book to your Kindle, first ensure [email protected] is added to your Approved Personal Document E-mail List under your Personal Document Settings on the Manage Your Content and Devices page of your Amazon account. Then enter the ‘name’ part of your Kindle email address below. Find out more about saving to your Kindle.
Note you can select to save to either the @free.kindle.com or @kindle.com variations. ‘@free.kindle.com’ emails are free but can only be saved to your device when it is connected to wi-fi. ‘@kindle.com’ emails can be delivered even when you are not connected to wi-fi, but note that service fees apply.
Find out more about the Kindle Personal Document Service.
To save content items to your account, please confirm that you agree to abide by our usage policies. If this is the first time you use this feature, you will be asked to authorise Cambridge Core to connect with your account. Find out more about saving content to Dropbox.
To save content items to your account, please confirm that you agree to abide by our usage policies. If this is the first time you use this feature, you will be asked to authorise Cambridge Core to connect with your account. Find out more about saving content to Google Drive.